Saturday, May 28, 2011

BARCELONA 3 MANCHESTER UNITED 1: KWA MARA NYINGINE BARCA YAIBURUZA MAN UNITED CHAMPIONS LEAGUE.

Kutoka kushoto Victor Valdes, Xavi na Erick Abidal wakishangilia mara baada ya kukabidhiwa Kombe la Klabu Bingwa ya Ulaya usiku huu katika Uwanja wa Wembley, Uingereza.

Wachezaji wa Barcelona wakishangilia bao lao la kwanza dhidi ya Manchester United.

Mshambuliaji wa Barcelona David Villa akipigilia  msumari wa mwisho katika jeneza la Man United bao ambalo lilizamisha ndoto za timu hiyo kunyakua ubingwa huo.

Mshambualiaji Leonel Messi akipiga shuti kali ambalo lilimshinda golikipa wa Man United Edwin Van de Sar na kutinga wavuni kuandika bao la pili la timu hiyo.

Messi akishangilia bao lake huku mabeki wa Man United wakiwa wamepigwa na butwaa.

Mshambualiaji wa Man United Wayne Rooney akifunga bao la kufutia machozi.

Van de Sar akiangalia mpira ukitumbukia nyavuni.

Mshambuliaji wa Man United Chicharito ambaye hakung'aa usiku wa leo akipambana na Valdes katika moja ya heka heka za mchezo huo.

Kocha wa Manchester United akiwapongeza wachezaji wa Barcelona kwa ushindi wao.

Nyota wa mchezo Xavi akiwa katika moja ya heka heka ambazo zilizaa bao la kwanza katika mchezo huo.

Rooney na Ryan Giggs wakiwa hawaamini kulipoteza kombe hilo kwa mara ya pili kwa Barcelona tena wakiwa nyumbani, mara nyingine ilikuwa ni fainali za mwaka 2009 zilizofanyika Rome, Italia.

No comments:

Post a Comment