MSHAMBULIAJI wa kimataifa kutoka nchini Cameroon, Samuel Eto'o anamatarajio kuwa timu yake ya zamani Barcelona itaifunga Manchester United kkatika mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya itayochezwa Jumamosi hii kkatika Uwanja wa Wembley.
Eto'o ambaye pia nachezea klabu ya Inter Milan sio mgeni sana na kombe hilo haswa ukizingatia kuwa ameshawahi kushinda kombe hilo mara mbili akiwa na Barca na moja akiwa na Inter.
Alishinda moja ya magoli dhidi ya Man United katika fainali zilizofanyika Rome, Italia 2009, na anatarajia kuwa historia inaweza kujirudia tena kwa timu yake hiyo ya zamani kunyakuwa kombe hilo tena.
"Nikitakuwa katika fainali hiyo nikiwa na imani kwasababu nina marafiki wazuri ambao watakuwa wanacheza hivyo moyo wangu utakuwa kwao," alisema Eto'o akihojiwa na mtandao wa UEFA.
"Moja kwa moja naipigia chapuo Barcelona kushinda. Lakini huwezi kujua kitu gani kitatokea. Wote Barcelona na Manchester United wana vikosi bora zaidi ukilinganisha na mwaka 2009. Naamini itakuwa ni fainali za kuvutia."
No comments:
Post a Comment