LONDON, England
KOCHA wa Arsenal Arsene Wenger anaamini kuwa wapenzi wa Uwanja wa Emirates hivi karibuni wataanza kumuona Nicklas Bendtner akifanya vitu vyake.
Bendtner (22), bado hajaanza kuonekana katika kikosi cha timu hiyo msimu huu ambapo anauguza maumuvu ya nyonga ambayo anaamini aliyapata baada ya kupata ajali ya gari Septemba mwaka uliopita, na kujitonesha katika Kombe la Dunia Afrika Kusini.
Hatahivyo, mshambuliaji huyo anaweza kuonekana katika kikosi cha timu hiyo kwa mara ya kwanza msimu huu, zaidi akiwa benchi la akiba katika mchezo dhidi ya Bimighham City baadaye, huku akiamini kuwa kuwa mchezaji huyo atakuwa fiti baada ya maumivu ya nyonga yaliyokuwa yakimkabili kwa kipindi cha miezi 12 iliyopita.
"Tusisahau kuwa toka Novemba mwaka uliopita Nicklas alitusaidia hapa na pale, lakini hakuweza kuonekana kutokana na maumivu," alisema Wenger.
"Tukiachilia ukweli kwamba alikwenda kwenye Kombe la Dunia hatujamuona Bendtner akiwa fiti katika kiwango chake kwa muda mrefu sana.
"Yuko karibu kurudi katika kiwango chake.
"Maumivu ya nyonga yalikuwa ni tatizo kwake, lakini sasa yameondoka."
No comments:
Post a Comment