Saturday, October 16, 2010

TOURE AWAOMBA WANASIASA NCHINI KWAO KUWA WATULIVU KATIKA KIPINDI HIKI CHA UCHAGUZI.

LONDON, England
BEKI wa Manchester City Kolo Toure mzaliwa wa Ivory Coast ametuma ujumbe wa maneno kwa wanasiasa wa nchi yake katika kipindi cha kuelekea uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Octoba 31, kuwaomba kuwa maslahi yao makubwa yawe kwa ajili ya watu wengi.

Katika mahojiano na gazeti la France Football Alhamisi, mchezaji huyo wa zamani wa Arsenal alisema anatarajia na haswa wanasiasa wa nchi yake siku zote kutoa kipaumbele kwa wananchi wakawaida.
"Bara letu la Afrika linakabiliwa na wakati mgumu hivi sasa. Nchi yangu Ivory Coast inakabiliwa na hekaheka uchaguzi wa Rais Octoba 31," alisema.

"lakini tunahitaji kuwapa watu pumzi ya hewa nzuri, na hilo linatakiwa kuanzia kwa wanasiasa ambao siku zote wana wajibu wa kufukiria uwingi wa watu wa kawaida kuliko kitu chochote. Ni muhimu kufanya hili kwa kizazi kijacho ambao wanatuona kama mifano, ukiwa kama mwanamichezo au mwanasiasa."

Kampeni za Urais zinaanza rasmi Ivory Coast Ijumaa, kampeni ambazo zitadumu kwa muda wa wiki mbili kabla ya uchaguzi wa kihistoria ambao labda unaweza kuliunganisha taifa hilo la Afrika Magharibi baada ya miaka mingi ya machafuko ya kisiasa.

Mchezaji wa Chelsea Didier Drogba, pia kutoka Ivory Coast, naye pia amewaomba wana siasa wa nchi hiyo kusaidia kurudisha amani ambayo ilikuwa imepotea kwa muda mrefu.

No comments:

Post a Comment