LONDON, England
MMILIKI wa kampuni wa New England Sports Venture (NESV) John W. Henry ameeleza hamasa aliyonayo baada ya kuinunua klabu ya Liverpool kwa paundi milioni 300.
Henry (61), ambaye pia anamiliki timu ya Baseball ya Boston Red Sox ya Marekani, alijitokeza wiki iliyopita, ambapo kulikuwa na vita ya kisheria baada ya wamiliki wa zamani wa kimarekani Tom Hicks na George Gillett kutaka kuing'ang'ania klabu hiyo.
"Zimekuwa ni siku za matukio, ya hapa na pale, zilikuwa zinachosha lakini hatimaye tumefanikiwa malengo na matarajio yetu," alisema Henry akiuambia mtandao wa klabu hiyo. "Najivunia timu ya watu ambao wamefanikisha mpango huu.
"Tumefurahi sana. Nikiwaongelea wote ninaoshirikiana nao huko Marekani, wote wamefurahi."
Hatimaye mpango huo ulikamilika rasmi Ijumaa mchana, hatahivyo kwa mujibu wa madai ya kisheria yaliyofunguliwa na Hicks na Gillett, Henry hakuwa na uhakika wa moja kwa moja kwamba kila kitu kitakwenda sawa na alikiri hilo katika kipindi cha mvutano kwamba alikuwa na wasiwasi kwamba NESV itanyimwa nafasi ya kuinunua klabu hiyo.
"Kuna siku nyingi nilikuwa nafikiria kama tutarudi nyumbani au hatutarudi mikono mitupu. Kwa ukweli, hata leo nilikuwa sina uhakika wa asilimia mia moja," alisema Henry.
"Kuna siku ambazo nilikuwa na uhakika lakini kulikuwa na vitu vingi vya hapa na pale hapa. Nilikuwa na watu makini ambao walifanya kazi nzuri ya katika kushughulikia hili na nina furaha limekwisha kwa mafanikio."
Mfanyabiashara huyo mzaliwa wa Illinois alifafanuwa kuwa kufanana kwa klabu hizo mbili ya Boston Red Sox na Liverpool ndiko kulikompelekea kufikia hatua ya kuinunua klabu hiyo ya kihistoria.
"Kuna vitu vingi vinavyofanana na ni kitu aambacho tumekuwa tukikijadili kabla ya kuanza harakati hizi. Tumegundua kuna mengi na mengi yanayofanana kati ya Liverpool 2010 na Red Sox ya 2001 walipoinunua.
"Kwa mfano tatizo la uwanja lilikuwa ni tatizo kubwa Boston mwaka 2001 na tulienda kule tukiwa hatujui la kufanya, kama tujenge uwanja mwingine au kuufanyia matengenezo uliokuwepo. Tuna tatizo kama hilo hapa.
"Tunatakiwa tusikilize, tujifunze, tuongee na jamii ya hapa, tuongee na baraza, tuongee na wanachama, lakini tatizo kubwa kuliko yote ni jinsi gani tutaifanya Liverpool iwe katika kipindi kirefu kijacho."
Kllabu ilipo hivi sasa ndani na nje ya uwanja, limekuwa tatizo na Henry anajua kwamba haitakuwa kazi rahisi kuiridisha timu hiyo kuendeleza ushindi kama ilivyokuwa zamani.
Aliendelea: "Kuna kazi kubwa ya kufanya kuirudisha klabu katika hadhi yake. Kiukweli kutokana na kazi tuliyofanya katika miezi miwili iliyopita, tumeona changamoto na matatizo yalijitokeza, na tutayafanyia kazi ili kuwaonyesha.
"Kuna vitu vikubwa vyenye umuhimu hapa nje na ndani ya uwanja na tunadhani tunaweza kuanzia kutoka hapo, lakini haiwezi kuwa rahisi. Tuna changamoto kubwa."
Wakati mashabiki wa Liverpool wakimkaribisha mmiliki mpya, hawakusita pia kuonyesha wasiwasi wao kwa mmiliki huyo mwingine wa kimarekani.
Kipindi Hicks na Gillet walipoinunua klabu hiyo 2007, ahadi walizotoa wamiliki hao hazikuwahi kutimizwa.
"Ilikuwa ni miaka mitatu migumu na kulikuwa na matarajio makubwa yaliyowekwa, hivyo kitu ambacho sitajaribu kufanya ni kuweka matarajio mengi," alikiri Henry
"Nataka kujenga matumaini kuliko kutimiza ahadi, Nikisema mimi, namaanisha 'New England Sports Ventures (NESV).
"Tuna kampuni yenye nguvu kifedha na vinginevyo tuna malengo mazuri ya kufikirika na tutaanza kuyafanya kazi kuanzi kesho."
"Tunachoweza kusema tutafanya kazi kwa bidii kwa ajili ya mashabiki wa Liverpool kwa kadri tunavyoweza na hatuna mashaka kuhusu hilo, kwani mnastahili," aliendelea Henry akiwaambia mashabiki wa Liverpool.
"Mmekuwa pamoja na klabu hii katika kipindi chote kigumu na tutafanya yote tunaweza kwa uwezo wetu wote kuwafanya mashabiki kujivunia klabu yao pamoja na sisi. Ni cgangamoto kubwa lakini nafikri tuko tayari kukabiliana nayo."
No comments:
Post a Comment