Sunday, October 17, 2010

MANCHESTER, CHELSEA ZANG'ANG'ANIWA, ARSENAL, TOTTENHAM, BOLTON ZAPETA.

MANCHESTER, Uingereza
MANCHESTER United jana iliendelea kuwaduwaza mashabiki wake nyumbani, baada ya kukubali sare ya mabao 2-2 dhidi ya West Bromwich Albion, katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.

Mchezo huo ambao ulichezwa kwenye uwanja wa Old Trafold ulishuhudia Mashetani Wekundu wakilazimika kupigana kulinda heshima na wageni wao ambao walionyesha soka safi kipindi cha pili.

Hadi kipindi cha kwanza kilipomalizika, Manchester United ndio waliokuwa wakiongoza kwa mabao 2-0 yaliyofungwa na Javier Hernandez na Louis Nani katika dakika za tano na 25 za mchezo.

Hata hivyo, West Bromwich Albion ambao wana rekodi ya kupanda na kushuka katika ligi hiyo walikuja juu na kulisaka lango la wapinzani wao na kufanikiwa kupata bao katika dakika ya 50.

Mpira huo uliotokana na adhabu iliyopigwa na mlinzi Chris Brunt, ulimgonga Patrice Evra na kujaa kimiani, ukimuacha mlinda mlango Edwin Van Der Sar akichupa bila mafanikio.

Wageni walifanikiwa kupata bao la pili katika dakika ya 55 kupitia kwa mshambuliaji
Somen Tchoyi ambaye alitumia makosa yaliyofanywa na Van Der Sar kuuweka mpira wavuni.

No comments:

Post a Comment