LONDON, England
ARSENE Wenger yuko tayari kumpa kibarua nahodha wa zamani wa Arsenal katika benchi lake la ufundi kama mmoja wa makocha kama nguli huyo atatundika daluga mwishoni mwa msimu huu.
Kiungo huyo anayechezea Manchester City kwa sasa alishakiri kuwa anaweza kutundika daruga zake mwishoni mwa msimu huu na Wenger atajaribu kwa mara ya pili kumchukua mchezaji huyo kama kocha, ilisema taarifa ya gazeti la The People.
Alijaribu kumsajili mchezaji huyo mwenye miaka 34 kama kocha mchezaji katika majira ya kiangazi 2009 lakini kiungo huyo alionekana kuvutiwa zaidi na Manchester City, akiamini kuwa atapata muda kucheza zaidi ili aweze kuitwa katika fainali za Kombe la Dunia 2010.
Hatahivyo Viera hakuweza kuitwa katika kikosi cha Ufaransa na amechezeshwa kidogo tu katika msimu huu huku akianza katika mchezo mmoja tu.
Hili limepelekea kufikia hatua hiyo wiki iliyopita kwamba kipindi chake cha kucheza soka kitakuwa kimefikia tamati.
No comments:
Post a Comment