LONDON, England
KIUNGO wa Arsenal Jack Wilshere amekiri kuwa alistahili kutolewa nje katika mchezo dhidi ya Birmigham Jumamosi lakini ameapa kuwa amejifunza kutokana na kosa hilo.
Kiungo huyo mchezeshaji alisema alikumbwa na dhahama hiyo dakika za majeruhi kabla ya mpira kumalizika katika Uwanja wa Emirates baada kumuinmgilia vibaya mshambuliaji wa Birmingham Nikola Zigic.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye miaka 19 amekuwa mkweli kwa tukio alilofanya.
"Nataka kusema kuwa nilidhamiria kumuingilia kwa nguvu Zigic na nakubali kuwa nilistahili kutolewa nje," alisema Wilshere akiuambia mtandao wa klabu hiyo.
"Sina chochote cha kupinga kuhusu kadi nyekundu niliyopewa na nitajifunza kutokana na hili. Nitakosa mechi tatu sasa kitu ambapo kinanisononesha, lakini nahitaji kusema nilistahili kadi nyekundu."
Wilshere sasa atakosa mechi tatu za nyumba kuanzia mchezo dhidi ya Manchenster City mwishoni mwa wiki inayokuja.
No comments:
Post a Comment