MILAN, Italia
RAIS wa Inter Milan Massimo Moratti amelirudia suala la Lionel Messi, lakini akisema kuwa hawezi kuvunja benki kumsajili mchezaji huyo.
"Messi? ni waandishi ndio wanaendelea kulikuza suala lake," alisema Moratti akiliambia gazeti la Sky Sport la Italia.
"Messi ni mchezaji anayehitajiwa na klabu yoyote, lakini nadhani ni zoezi gumu sana.
"Huko mbele? Nani anaweza kujua..."
Moratti alihamishia maongezi hayo ya kuhusiana na na kumsajili Messi, kwa kuelezea ushindi mwembamba waliopata dhidi ya Cagliari Jumapili.
"Nimependa kikosi kilichocheza dhidi ya Cagliari, walionyesha morali ambao huku unahitajika katika mchezi kama hizo," alisema Moratti.
"Sidhani kama tunamtegemea Eto'o, walisema hivyo wakati tuko na Zlatan Ibrahimovic, lakini tumeshinda mataji mawili ya ligi.
No comments:
Post a Comment