Monday, October 18, 2010

EDUARDO: KUVUNJIKA MGUU KULICHANGIA KUPOROMOSHA KIWANGO CHANGU.

SHAKHTAR, Ukraine
MSHAMBULIAJI wa Shakhtar Donetsk Eduardo amesema kuwa kitendo cha kuvunjika mguu kilichangia kutokurudi katika kiwango chake wakati alipokuwa Arsenal.

Eduardo (27) aliumia mwaka 2008 baada ya kuchezewa vibaya na mchezaji wa Birmingham City Martin Taylor. Baada ya kupigania kiwango chake na afya yake, aliruhusiwa kuhamia kwa mabingwa wa Ukraine katika kipindi cha majira ya kiangazi.

Akiongea na Skysports.com, Eduardo alifafanua kuwa anachotilia maanani ni kupata matokeo mazuri Jumanne usiku katika mchezo wao wa Champions League kuliko kuchukuliwa na hisia zangu.

"Sikukusudia kuvunja mguu wangu, lakini ni kweli naweza kusema kuwa tukio lilitia doa soka langu," alisema Eduardo.

"Siwezi kujua ni kitu gani kingenitokea kama nisingeumia, lakini pengine ningeendelea ningekuwa bado katika timu.

"Kama nitacheza nitakuwa na hisia kali, lakini nitajaribu kutilia maanani mchezo huo na nitakuwa nimetulia katika mechi hiyo.

"Shakhtar Donetsk inakuja London kwa utulivu kwa ajili ya mchezo wao mgumu.

"Tumeshinda michezo miwili iliyopita na hatuna wasiwasi. Haitakuwa rahisi, lakini tunataka kuwashangaza."
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Croatia aliongeza: "Nahitaji kukumbukwa kwa kuwa mchezaji mzuri uwanjani na sio mambo yaliyopita wakati niko Arsenal, Ingawa naenda katika mchezo huu nikiwa sina cha kulipiza.

"Mashabiki siku zote wako nyuma yangu na wako katika moyo wangu na bado nawasiliana na Denilson, Cesc Fabrigas na Robin [van Persie]."

No comments:

Post a Comment