Monday, October 18, 2010

MAJINA YA WATAKAOWANIA TUZO ZA MCHEZAJI BORA AFRIKA KUTANGAZWA NOVEMBA.

CAIRO, Misri
KATIBU MKUU wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF) Hicham El Amrani amesema kuwa majina ya watakaowania tuzo za mchezaji bora wa shiriki hilo kwa mwaka huu yanatarajiwa kutangazwa katika wiki ya kwanza ya Novemba.

"Orodha yoyote iliyotoka hivi haijatoka kwetu," alisema Amrani. "Tunakwenda kwa mujibu wa ratiba. Tunachukua mashindano yote yaliyofanyika 2010 kuanzia ngazi vilabu na timu za Taifa ikijumuisha michuano ya Mataifa ya Afrika yaliyofanyika Angola na Kombe la Dunia la South Afrika."

El Amrani alisema kuwa tayari majina ambayo yatakuwa yamegawanjika katika sehemu mbili yaani majina ya wachezaji wa mwaka ambao wanacheza Ulaya na majina wachezaji wa mwaka ambao wanacheza katika ligi za hapahapa Afrika yameshawasilishwa katika kamati ya ufundi na maendeleo pamoja kamati ya habari ya CAF kwa ajili ya uhakiki. Kamati hizo zinatarajiwa kufikisha kuchuja majina hayo na kubakia kumi kwa ajili ya tuzo za wachezaji wa nyumbani na matano kwa ajili ya wachezaji wa nje.

Alisema majina hayo yatapunguzwa zaidi na kufikia matatu kila upande, baada ya vyama vya soka 53 vya Afrika watapopiga kura kwa ajili ya uteuzi wa mwisho.

Sherehe hizo zinatarajiwa kufanyika wiki ya tatu ya mwezi Desemba lakini mahala itakapofanyika bado hapajaamuliwa.

No comments:

Post a Comment