Wednesday, October 20, 2010

INTER YAPIGA NNE, LYON, MANCHESTER UNITED, BARCELONA NAZO ZAPETA.

MILAN, Italia
TIMU ya Inter Milan jana iliendeleza ubabe katika kundi A baada ya kupata ushindi wa tatu katika kundi hilo kwa kuidhibu bila ya huruma Tottenham Hotspurs kwa mabao 4-3.

Inter ambao katika mchezo wao wa kwanza walifanikiwa kuwafunga Werder Bremen nyumbani kwa mabao 4-0, walifanikiwa kuwadhibiti Spurs katika kipindi cha kwanza ambapo mpaka kinamalizika walikuwa tayari wameshashinda mabao 4-0 mabao yaliyofungwa na Javier Zanetti, Samuel Eto'o na Dejan Stankovic huku mabao ya Tottenham yote yakifungwa na Gareth Bale katika kipindi cha pili na kuifanya timu hiyo iendelee kubaki nafasi ya pili wakiwa wamezidiwa pointi na Inter wanaoongoza kundi hilo na pointi mbili zaidi ya FC Twente na Bremen ambao walitoka sare ya bao 1-1.

Jumanne usiku tulishuhudia FC Bayern Munich, Chelsea, Real Madrid na Arsenal wote wakijizolea pointi katika makundi yao na kufikisha tisa, jana likuwa ni zamu ya Olympique Lyon, ambao walishinda mabao 2-0 dhidi ya Benfica ukiwa ni mchezo wao wa tatu kushinda katika Kundi B, Schalke 04 wanakamata nafasi ya pili baada ya kuifunga timu ambayo haina pointi ya Hapoel Tel Aviv kwa ambao 3-1.

FC Kobenhavn haijapoteza pointi katika kundi D kabla ya jana usiku kwani walipoteza baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Barcelona mabao yaliyofungwa na Lionel Messi. FCK inazidiwa na barcelona kwa pointi moja lakini inawazidi kwa pointi tano na nne Rubin Kazan na Panathiniakos baada ya jana timu hizo kutoshana nguvu kwa kutofungana.

Uwezo binafsi uliofanywa na Nani dakika ya saba ulitosha kuifanya Manchester United kuibuka kidedea kwa kuifunga timu ya Bursaspor bao 1-0 katika uwanja wa Old Trafordna kuifanya iongoze kundi D kwa tofauti ya pointi mbili dhidi ya Rangers ambayo ndio inayofuatia baada ya kulazimishwa suluhu na ya bao 1-1 dhidi ya Valencia.

No comments:

Post a Comment