Wednesday, October 20, 2010

RIJKAARD ATUPIWA VIRAGO GALATASARAY.

UONGOZI wa Galatasaray ya Uturuki umeamua kumtupia virago kocha wake Frank Rijkaard baada ya klabu kuanza vibaya ligi ya msimu wa 2010-11.

Taarifa ya katika tovuti ya klabu ilisema kuwa mkataba wa kocha huyo wa zamani wa Barcelona umesitishwa, pamoja na msaidizi wake Johan Neekens naye ameiacha klabu hiyo.

Kwa sasa klabu hiyo inashikilia nafasi ya tisa katia msimamo wa ligi kuu ya nchi hiyo katika mechi nane ilizocheza wakiwa wamejikusanyia pointi 12 mpaka sasa na wakiwa nyuma ya pointi nae dhidi ya vinara wanaoongoza ligi hiyo Bursaspor.

Rijkaard (48) alichukua kibarua cha kuinoa klabu hiyo 2009, lakini alishindwa kuipa mafanikio klabu hiyo kwani walimaliza ligi msimu uliopita wakiwa nafasi ya tatu.

No comments:

Post a Comment