LONDON, England
MSHAMBULIAJI wa Manchester United Wayne Rooney ametoa taarifa ya kuthibitisha nia yake ya kuondoka Old Traford.
Mchezaji huyo wa zamani wa Everton alielekeza kuwa maamuzi yake yametokana na ukweli kwamba bodi ya klabu hiyo imeshindwa kumuhakikishia kama wanampango wowote wa kununua wachezaji zaidi ili kuboresha kikosi hicho.
"Nilikutana na David Gill wiki iliyopita na hakunihakikishia chochote kuhusu kuboresha kikosi siku zijazo," alisema Rooney.
"Ndio nilipomwambia kuwa sitasaini mkataba mpya."
Rooney pia amekiri kuvutiwa na kushangazwa na kauli ya Sir Alex Ferguson aliyosema Jumanne alipoongea na vyombo vya habari, ambapo Mscotland huyo alisema "ameshtushwa" na 'ameangushwa" na uamuzi aliochukua Rooney (24), lakini atabakia kuwa mchezaji anayempenda .
"Nilivutiwa kumsikiliza kitu gani atasema Ferguson jana na nilishangazwa na baadhi ya vitu alivyosema," aliendelea Ferguson.
"Ni ukweli mtupu aliosema, kuwa wakala wangu na mimi tulifanya mikutano mingi kuhusiana na mkataba mpya. Katika kipindi hicho tulipokutana nilitaka kuhakikishiwa kuhusu mwenendo wa klabu katika kuwavutia wachezaji nyota duniani.
"Sijawahi kuwa na chochote zaidi ya kuiheshimu MUFC. kwanini nisiiheshimu kwani imekuwa na historia ya kipikee na haswa miaka sita iliyopita ambayo nimekuwa na bahati ya kuwa nayo?
"Kwa mimi hakuna kingine zaidi ya kushinda vikombe kama klabu ilivyofanya chini ya Sir Alex. kwasababu ya hilo nadhani swali niliulizwa litakuwa limejibiwa."
No comments:
Post a Comment