MADRID, Hispania
BEKI wa zamani wa Real Madrid Roberto Carlos amekiri katika mahojiano yake na gazeti la L'Equipe kuwa Zinedine Zidane ni mchezaji aliyepata kumuona katika maisha yake.
Akijulikana zaidi kwa staili yake ya kwenda kushambulia akitokea nyuma upande wa kushoto na mashuti aliyokuwa akipiga katika mipira ya adhabu (free kicks), Mbrazil huyo alimtaja mchezaji mwenzake huyo kuwa ni bora katika kipindi chake chake cha uchezaji soka na hata baadae, akifafanua kuwa ni bahati kwamba walicheza pamoja katika kikosi cha Madrid.
"Ni mchezaji bora niliyepata kumuona," alisema Rorbeto Carlos. "Ronaldo alimkuwa mzuri, lakini Zizou alikuwa na kitu cha ziada. kucheza pamoja naye ilikuwa ni kitu cha kufurahisha! Mashabiki walikuwa wakiwasili mapema Bernabeu ili kumuona akipasha misuli!"
Zidane alianza kujulikana katika ulimwengu wa soka baada kuonyesha kiwango bora katika fainali za Kombe la Dunia zilizofanyika Ufaransa 1998 katika mchezo dhidi ya Brazil, ambapo alifunga mabai mawili, na Champions League, wakati alipofunga bao la kukumbukwa na kuisaidia Mdrid kunyakuwa taji la tisa.
Kwa sasa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 38 ni mmoja wa viongozi wa klabu hiyo.
No comments:
Post a Comment