Friday, October 8, 2010

BRAZIL YAIADHIBU IRAN.

ABU DHABI, Falme za Kiarabu
DANIEL Alves, Alexandre Pato na Nilmar, juzi waliifungia Brazil mabao matatu katika mchezo wa kihistoria dhidi ya Iran ambapo kigogo hicho kilishinda 3-0.
 
Mchezo huo uliokuwa maalumu kwa ajili ya maonyesho, ulimpa raha kocha mpya wa Brazil,
Mano Menezes ukiwa ni ushindi wake wa pili mfululizo tangu alipochukuwa nafasi ya Carlos Dunga.
 
Dunga, nahodha wa zamani wa Brazil, alitupiwa virago muda mfupi baada ya kutolewa katika fainali za Kombe la Dunia 2010 nchini Afrika Kusini.
 
Alves alianza kufunga bao dakika 14 kwa mpira wa adhabu kabla ya Pato kuongeza dakika 69. Nilmar alifunga bao la tatu dakika mbili kabla ya mchezo kumalizika.
 
Brazil itavaana na Ukraine Jumatatu ijayo katika mchezo wa kirafiki utakaopigwa mjini Derby, England, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya michuano ya Kombe la Amerika majira ya kiangazi.

No comments:

Post a Comment