ACCRA, Ghana
NAHODHA wa zamani wa Ghana, 'Black Stars', Stephen Appiah amesema anataka kuifundisha
timu ya taifa ya nchi hiyo baada ya kustaafu soka.
timu ya taifa ya nchi hiyo baada ya kustaafu soka.
Kauli ya kiungo huyo wa kimataifa aliyewahi kung'ara na klabu za Ulaya, imekuja muda mfupi baada ya kustaafu kuitumikia Black Stars.
"Nina kiu ya kuinoa Ghana baada ya kustaafu soka, lakini sasa naelekeza nguvu katika klabu yangu ya Cesena. Tutaona siku za usoni nini kitatokea," alisema Appiah.
Kiungo huyo alidai siyo lazima kuinoa timu ya wakubwa lakini pia atakuwa radhi kuanza nafasi ya kocha msaidizi au yoyote atakayopewa na Shirikisho la Soka Ghana (GFF) muda wake ukifika.
Appiah (29), alisisitiza kamwe hatarejea kucheza soka ya kimataifa baada ya kutundika daluga Agosti, mwaka huu na kuongeza kuwa ameridhika kuiongoza Ghana katika fainali mbili za Kombe la Dunia.
Alisema amefikia uamuzi huo ili kutoa nafasi kwa wachezaji chipukizi kuitumikia Ghana katika michuano mbalimbali.
Baadhi ya wachezaji nguli waliowahi kuvuma na kikosi cha Black Stars ni Abedi Pele, Tony Yeboah, Gargo Mohammed, Osei Kufuor, Augustine Arhinful na Yaw Preko.
No comments:
Post a Comment