LONDON, England
RIO Ferdinand siyo tu anahaha kulinda nafasi yake ya unahodha, lakini pia anapasua kichwa kuhakikisha anapata namba kikosi cha kwanza cha England.
Maumivu ya goti yamemuweka nguli huyo katika hali ngumu baada ya kukosa fainali za Kombe la Dunia 2010. Nafasi yake ilichukuliwa na msaidizi wake Steven Gerrard.
Nahodha huyo wa Liverpool, alisema atakuwa radhi kurudisha kitambaa cha unahodha kwa Ferdinand baada ya kupona.
Ferdinand amerejea uwanjani kwa kishindo baada ya kupona majeraha ya goti na tayari ameanza kuingiwa hofu ya kupokwa namba na kinda wa Everton, Phil Jagielka aliyecheza mechi mbili za kufuzu fainali za Kombe la Ulaya.
Jagielka alisimama 'mkoba' katika mechi ambazo England ilishinda mabao 4-0 dhidi ya Bulgaria kabla ya kuifumua Uswis mabao 3-1. Fabio Capello anaweza kumtumia chipukizi huyo katika mchezo wa Jumanne ijayo dhidi ya Montenegro.
Jagielka alikuwa mchezaji pekee aliyecheza dakikika zote 90 katika mechi hizo. Licha ya kurejea uwanjani, Capello ana hofu kama mkongwe huyo (31) yupo katika kiwango bora kwa ajili ya mechi za kufuzu Kombe la Ulaya.
No comments:
Post a Comment