LONDON, England
MMILIKI mtarajiwa wa klabu ya Liverpool, John Henry amepanga kukutana uso kwa uso na mshambuliaji wa timu hiyo Fernando Torres.
Bilionea huyo anayemiliki klabu ya mchezo wa 'baseball' ya Red Sox huenda akawa bosi mpya wa Liverpool wiki ijao. Henry anataka kuinunua klabu hiyo ingawa anakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa mmiliki Tom Hicks.
Hicks amepeleka pingamizi mahakamani akipinga Liverpool kuuzwa kwa pauni milioni 300 (sh. bilioni 690), lakini Henry anayeungwa mkono na kundi la wachezaji anapewa nafasi kubwa kutua Anfield.
Henry amepanga kukutana na Torres haraka kuzungumzia mustakabali wake baada ya nyota huyo kuwa katika hali ngumu kufuatia majeraha ya korodani yanayomuandama muda mrefu tangu msimu uliopita.
Torres anatarajiwa kurejea uwanjani katika mchezo ambao Liverpool itavaana na Everton katika mchezo wa ligi uliopangwa kuchezwa kesho. Liverpool ipo nafasi ya 18 katika katika msimamo wa ligi ikiwa na pointi sita.
No comments:
Post a Comment