Thursday, October 7, 2010

MASHABIKI WA TUNISIA JELA MISRI.

CAIRO, Misri
MASHABIKI wa soka 11 raia wa Tunisia wamefungwa jela baada ya kutokea vurugu katika mchezo ambao Esperance ilichapwa mabao 2-1 ilipovaana na Al Ahly ya Misri.
 
Katika mchezo huo wa nusu fainali kuwania Kombe la Orange, mashabiki wa Esperance walipata hasira baada ya mechi hiyo kumalizika ambapo walidai mabao ya Al Ahly hayakuwa halali.
 
Jaji wa mahakama wa jiji la Cairo, aliwahukumu jela mashabiki 11 kwa madai ya kufanya fujo baada ya pambano hilo kumalizika. Ilidaiwa mashabiki wa Tunisia walipigana na askari wa Cairo.
 
Polisi wa Cairo walishindwa kudhibiti hasira za mashabiki wa Tunisia ambao walipinga uamuzi katika mchezo huo. Hali ya uwanja ilikuwa mbaya zaidi kabla ya maofisa usalama kuingilia kati kuokoa jahazi.
 
Mashabiki wenye hasira waliwavamia polisi na kutoa kipigo. Polisi 11 walikimbizwa hospitali kwa ajili ya matibabu kabla ya kuruhusiwa. Mashabiki wawili wa Tunisia walipandishwa ndege kurudishwa nyumbani.
 
Shirikisho la Soka Afrika (CAF) linafanya uchunguzi wa kuhusiana na tukio hilo ambalo litajadiliwa na Kamati ya Maadili kabla ya kutolewa uamuzi baada ya kupitia kwa kina vielelezo.

No comments:

Post a Comment