YAOUNDE, Cameroon
WACHEZAJI wa Cameroon na Kongo watapewa chanjo za kuzuia maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu kabla ya timu hizo kuvaana kesho katika mchezo wa kufuzu fainali za Mataifa Afrika 2012.
Mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka, unatarajiwa kuchezwa Kaskazini mwa Cameroon katika mji wa Garoua, uliokumbwa na maambukizi ya ugonjwa huo hatari kwa miezi kadhaa.
Chama cha Soka Cameroon (FA) kilisema kikosi cha Cameroon kiliwasili Garoua Jumanne iliyopita kiliondoka Jumatano asubuhi kwenye Hoteli ya Benoue na jana walipatiwa vidonge vya kuzuia maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu.
"Tuliambiwa na Wizara ya Afya hali ya ugonjwa wa kipindupindu ni kubwa, lakini tupo makini sana tumechukua tahadhari kwa wachezaji wote kupimwa na watakuwa sehemu moja maalumu kabla ya Jumamosi kucheza mchezo huo," alisema mmoja wa madaktari wa Cameroon.
Kwa mujibu wa FA, wachezaji wa Kongo watahusika na utaratibu huo. Kocha wa timu ya taifa ya Kongo, Robert Nouzaret alitaka mchezo huo uhamishwe kutoka jiji la Yaounde kwenda Garoua ombi ambalo lilikubaliwa.
No comments:
Post a Comment