Thursday, October 7, 2010

SHEVCHENKO KUTIMIZA MECHI YA 100 UKRAINE.

NYOTA wa zamani wa klabu ya AC Milan na Chelsea Andriy Shevchenko anatarajiwa kuwa mchezaji wa kwanza wa Ukraine kucheza mechi 100 wakati timu hiyo itakapocheza na Canada, Ijumaa.

Mshambuliaji huyo alianza kuichezea timu hiyo miaka 15 iliyopita katika mchezo wa kutafuta tiketi ya kufuzu michuano ya Ulaya 1996 dhidi ya Croatia na mchezaji huyo mzoefu bado hapendi kukumbuka mechi hiyo. Hatahivyo na hayo Chevchenko anazo kumbukumbu nyingi za kukumbukwa na timu hiyo.

Hakuna kitu kibaya kama tulivyofungwa mabao 4-0. Nataka nikumbuke mambo mazuri na nashukuru kwamba yapo mengi katika miaka 16 niliyochea timu hiyo," alikaririwa Chevchenko na tovuti ya uefa.com.

"Kampeni zetu za Kombe la Dunia mwaka 2006 bado ziko nazikumbuka, haswa pale Ukraine ilipopoteza michezo yake mitatu katika hatua za mwanzo katika kutafuta nafasi ya kuvuzu. Nakumbuka mchezo wetu dhidi ya Uturuki wakati mashabiki wa nyumbani walipotuzomea haya mambo huwa yanakatisha tamaa.

"Tulichemka kwenda katika Kombe la Dunia lililopita lakini sasa tunajiandaa na michuano ya Ulaya 2012 tukiwa na nguvu za ziada. Naamini nitakuwa fiti kwenye michuano hiyo na nitatumia nguvu zangu zote pamoja na uzoefu nilionao kuhakikisha timu inafanikiwa hapa nyumbani. kwasasa nitakosa baadhi ya mechi za kufuvu, hatahivyo tunawapa umuhimu marafiki zetu na tunajaribu kucheza kwa kiwango bora.

"Kufikisha michezo 100 ni safari ndefu, hata kwa wale, kama mimi, ambao huwa hawafuatilii mambo ya uwiano."

No comments:

Post a Comment