Thursday, October 7, 2010

"HATUMTEGEMEI XAVI," - MARCHENA.

MADRID, Hispania
MCHEZAJI wa kimataifa wa Hispania Carlos Marchena amesisitiza kikosi cha timu ya Taifa ya nchi hiyo hakimtegemei kiungo mchezeshaji wa timu hiyo Xavi, wakati wakijiandaa kucheza na Lithuania na Scotland bila nyota huyo wa Barcelona.

Beki huyo mzoefu ambaye alikuwemo katika kikosi hicho wakati kilipobeba Kombe la Ulaya 2008 pamoja na Kombe la Dunia 2010, anaamini kuwa kuna wachezaji wengi ambao wanaweza kuziba pengo la mchezaji huyo wa katikati.

"Ni matarajio yetu kuwa hatutamtegemea mchezaji huyo. Ni mchezaji mzuri lakini wako wengine pia ambao wanaweza kucheza nafasi yake na wako tayari kuchukua nafasi yake," alisema Marchena.

"Ni lazima tuendeleze ushindi na kucheza mchezo wa kuvutia. Soka ndivyo lilivyo huwa inatokea, mnapoteza mchezo muda mwingine. Tunachotakiwa ni kugundua makosa yetu na kuhakikisha hayajirudii tena."

No comments:

Post a Comment