LONDON, England
MCHEZAJI mpya wa Chelsea Ramires amekiri kuwa tatizo kubwa linalomkumba kwasasa ni lugha ya Kiingereza.
Ramires (23), alisajiliwa kutoka Benfica katika msimu wa majira ya kiangazi na alianza katika mchezo wa wiki iliypita dhidi ya Arsenal ambapo timu hiyo ilishinda mabao 2-0. Baada kuhamia katika nchi ambazo zinaongea lugha ya kireno ambayo ndio lugha ya nyumbani, kiungo huyo alisema kuwa mawasiliano na wachezaji wenzake yalikuwa tatizo kubwa na wachezaji wenzake katika miezi ya mwanzo alipotua Stamford Bridge.
Akiongea na gazeti la Daily Star, Mbrazil huyo alisema: "Bado sijaweza kabisa lakini najaribu. Jambo kubwa gumu linalonikabili ni lugha.
"Wakati mwingine unahitaji kuongea na mtu unakuwa huwezi au huelewi lakini nadhani nitaweza baadae."
No comments:
Post a Comment