MADRID, Hispania
KOCHA wa Real Madrid Jose Mourinho amejibu maswali ya watu kuhusu ni mchezaji gani anayeona ni bora duniani, na kumchagua mchezaji wake Cristiano Ronaldo kuwa namba moja.
Bosi huyo Mreno alikuwa akihijiwa na Telemadrid kuhusu maendeleo ya mpango kwa klabu hiyo, na mawazo yake ya nani anamuona ni mchezaji bora kati ya Messi na Ronaldo.
Akiwalinganisha wote wawili, Mourinho alijibu, "Kuna machaguo mawili - Cristiano, and Messi. Kama ukimchagua Cristiano kuwa namba moja, basi Messi atakuwa wa pili. Lakini kwangu mimi Cristiano ni namba moja."
Kocha huyo wa zamani wa Chelsea pia alisema kama kuna kitu chochote ambacho angependa kushinda katika msimu huu, angependa zaidi kuwa kocha wa kwanza kutetea ubingwa wa Champions League katika msimu huu baada ya kulichukua akiwa na Inter msimu uliopita.
"Champions League ni shindano la mashindano. Ni muhimu zaidi na makubwa kutokana na ubora wake.
"Sitaki nionekane kama mjinga, lakini nahitaji ubingwa wa Champions League kwa huu kwa sababu nahitaji kutetea ubingwa wangu, lakini pia kupeleka ubingwa huo Real Madrid ambapo unatakiwa uwe."
No comments:
Post a Comment