Monday, October 11, 2010

"SIWEZI KUWA KAMA FERGUSON AU RIJKAARD," - LARSSON.

LANDSKRONA, Sweden
MCHEZAJI nyota wa Zamani wa Sweden, Celtic, Barcelona na Manchester United Henril Larsson ambaye siku zote alikuwa akidai kazi ya ukocha haimvutii baada ya kuacha kucheza mpira, lakini sasa mshambuliaji huyo wa zamani ameonyesha kufurahia nafasi yake ya ukocha katika klabu ya Landskrona.

"Ni kweli nilikuwa sitaki kuwa kocha kabisa, lakini wakati umri ukiwa mkubwa unagundua kuwa ni vizuri kuliko ulivyokuwa ukifikiri mwanzoni. Unaona picha yote kwa usahihi kuliko ulivyokuwa ukiona ulivyokuwa mdogo na napenda mpira," alisema Larsson akiuambia mtandao wa fifa.com.

"Kuwa kocha ni maamuzi magumu mwishini. Na nafurahia. Kuna kipindi kizuri na kibaya na inaweza kukuchanganya, lakini pia nilikuwa nikichanganyikiwa kipindi fulani nilipokuwa nacheza."

Larsson amefanya kazi na makocha wengi katika kipindi chake cha uchezaji, lakini hakuna kocha hata mmoja ambaye anafanana na jinsi Larsson anavyofundisha.

"Nikuwa na bahati sana kucheza chini ya makocha wengi wazuri na kitu kitu ambacho nimekuwa nikifanya ni kudokoa machache kutoka kwa wote hao walionifundisha ambayo yanaweza kunisaidia. Katika mpira hakuna jipya, ni vitu vinavyoendelea kwa miaka mingi, hivyo siwezi kusema nitafanya kitu ambacho hakijawahi kufanywa hapo kabla.

"Kitu unachoweza kufanya ni kuwa mwenyewe. Hata nikijaribu, siwezi kuwa kama [Sir Alex] Ferguson, siwezi kuwa kama [Martin] O'Neil na siwezi kuwa kama [Frank] Rijkaard. nataka niwe mimi mwenyewe, na wa aina ya peke yangu, na hicho ndicho nachojaribu kufanya."

No comments:

Post a Comment