Monday, October 25, 2010

PELLEGRINI: ULIKUWA NI UAMUZI MGUMU KUMUACHA RAUL.

VALPARAISO SANTIAGO, Chile
KOCHA wa zamani wa Real Madrid Manuel Pellegrini amezungumzia magumu aliyokutana kuhusu kumwanzisha mshambuliaji mkongwe katika kikosi chake katika kipindi alichukuwa akifundisha klabu hiyo.

Kocha huyo raia wa Chile alikuwa na wakati mgumu msimu uliopita wakati timu ilipomaliza katika nafasi ya pili nyuma ya Barcelona kwa mwaka wa pili, na kuchukua majukumu ya kumuacha mchezaji huyo katika kikosi hicho, zaidi kwa ajili ya maendeleo ya klabu hiyo.

Hatahivyo, katika mahijiano yake na gazeti moja la Chile, bosi huyo wa zamani wa Villareal alisema kwamba ilikuwa ni lazima kumuacha ingawa kulikuwa na mawazo tofauti, na pia alifurahia kufanya kazi na Cristiano Ronaldo.

"Ilikuwa ni vigumu kwangu kumwacha Raul, na maamuzi niliyochukua yalikwenda kinyume na baadhi ya viongozi. Ingawa mchezaji siku zote alielewa.

Cristiano anajali shughuli yake. Anapenda mpira, na pia anapenda vyombo vya habari. Tulikuwa na kundi la wachezaji wazuri, lakini Madrid sio klabu am,bayo iko tayari kwa mipango. Kama ningeendelea mwaka huu tungekuwa tuko vizuri."

Pellegrini pia alisema bado anaendelea kuwa na mahusiano mazuri na Mkuregenzi Mkuu Jorge Valdano na anamatumaini kocha wa sasa Jose Mourinho atapatiwa kila kitu kinahitajika ili afanikiwe.

Aliongeza: "Huwa naongea mara kwa mara na Jorge Valdano, na tuna mahusiano mazuri, sitaki nichambue kazi anayofanya Mourinho, lakini napenda nimtakie kila la heri."

No comments:

Post a Comment