BARCELONA, Hispania
KOCHA wa Barcelona Pep Guardiola amedai kuwa mpinzani wake Jose Mourinho anaweza kuwa kocha bora katika dunia, na kwamba Real Madrid "wana timu nzuri".
Kocha huyo alikuwa akijibu maswali leo kuhusu mechi inayowakabili ya Copa del Rey utakaochezwa Jumanne jioni dhidi ya AS Ceuta wakati alipoulizwa maoni yake kuhusu Mourinho, na jinsi gani alivyoitengeneza timu yake.
Guardiola alisema: "Pengine ni kocha bora duniani. Mara nyingi ni vigumu kuamua katika kesi hizi kwamba ni nani bora, lakini kazi yake katika nchi kadhaa ni safi. Real Madrid wana timu nzuri, na mimi nilijua kuwa ligi ya msimu huu itakuwa na ushindani kutoka mchezo wa kwanza. Tunatarajia tutajitahidi kuwa juu. "
Bosi huyo baada ya hapo alihamishia maongezi katika mchezo wao huo unaokuja dhidi ya timu hiyo ya daraja la pili ambayo imepakana na pwani ya Afrika Kaskazini, na kuwa na waiswasi jinsi gani mchezo huo unavyoweza kuwa mgumu kama wachezaji wake wasipokuwa makini.
Aliendelea: "Hatutakiwi kuwa wavivu. Nina imani kubwa katika timu, na tuna nia ya kushindana. Kuna wachezaji katika kikosi wenye sifa kamilifu kwa ajili ya mchezo huu. Tunahitaji miguu safi na kuna wachezaji ambao wana desturi ya kucheza mechi dhidi ya timu za Sirie B na kushuka chini. Unaweza kuwa sio mchezo muhimu kwao, lakini ni mchezo hatari kwetu.
"Timu yetu kamwe huwa hatuwadharau wapinzani wetu, na hatuwezi kufanya hivyo kwa Ceuta, ambapo kuna mashabiki wengi wa Barcelona. Naelewa kwamba wanataka kuwaona Xavi [Andres] Iniesta au Leo [Messi], lakini hii timu ina wachezaji wengi wazuri. "
No comments:
Post a Comment