Wednesday, October 27, 2010

PWEZA PAUL AFARIKI DUNIA.

PWEZA maarufu aliyekuwa akitabiri mechi za michuano ya Kombe la Dunia, ajulikanaye kama Paul amefariki dunia.


Mbali na kutabiri kwamba Hispania itaifunga Uholanzi katika mchezo wa fainali, Paul pia alitabiri kwa usahihi michezo saba ambayo timu ya Ujerumani ilicheza katika michuano hiyo. Kiwango ambacho kiliongezeka ikilinganishwa na rekodi yake ya kawaida, ambayo alitabiri matokeo yaliyo sahihi manne ya michuano ya Ulaya 2008.


Baada ya michuano hiyo iliyofanyika Afrika Kusini, Pweza huyo alitabiri Uingereza itakuwa nchi ambayo itandaa michuano ya Kombe la Dunia 2018, kabla ya kurudia katika kazi yake ya kawaida katika kituo cha Sea Life Oberhausen Aquariuam, Ujerumani.


"Uongozi na wafanyakazi wa kituo cha Oberhausen Sea Life walishtushwa baada ya kugundua Pweza Paul ambaye alijizolea umaarufu mkubwa duniani katika KOmbe la Dunia, kwamba alifariki dunia usiku," ilisema taarifa ya aquarium.

No comments:

Post a Comment