Wednesday, October 13, 2010

UEFA YAANZA UCHUNGUZI WA MECHI ILIYOVURUGIKA KATI YA ITALIA NA SERBIA.

SHIRIKISHO la Soka Ulaya (UEFA) limethibitisha kuwa limeunda kamati maalumu ya uchunguzi wa tukio lilitokea jana kati ya Italia na Serbia na kusababisha mchezo huo wa kutafuta tiketi za kufuzu michuano ya Ulaya kuvunjika.

"Kutokana na tukio la jana la mechi baina ya Italia na Serbia katika Uwanja wa Luigi Ferraris, Genoa baada ya dakika sita za mchezo huo zilizochezwa, UEFA imeanza kufanya uchunguzi mara moja kupitia kamati yake ya nidhamu kwa tukio lilishuhudiwa na jana na mazingira yake," ilisema taarifa ya UEFA.

"Mara taarifa itakapokamilika, wakisaidiana na ripoti ya waamuzi na makamisaa, suala hilo litapelekwa kamati ya nidhamu ya UEFA ambao watalipitia na kulitolea maamuzi.

No comments:

Post a Comment