Wednesday, October 13, 2010

"TULISTAHILI USHINDI TULIOPATA." - CUPERLY.

KOCHA wa timu ya Morocco Dominique Cuperly ameuambia mtandao wa timu hiyo kwamba timu yake ilistahili ushindi wa bao 1-0 iliyoupata dhidi ya Tanzania mwishoni mwa wiki iliyopita Dar es Salaam. Alisema wachezaji wake ndio wanaostahili kupongezwa na pointi tatu walizochukua zinaonyesha ubora wao, haswa baada ya kikosi hicho kupoteza pointi mbili nyumbani katika mchezo wao wa kwanza dhidi ya Afrika ya Kati.

"Ushindi huu unawarudia wachezaji. kwani tumepata kitu tulichokuwa tunakitafuta. Pointi tatu hizi tulizopata ugenini zitakuwa na umuhimu katika mashindano yote. Tutauhifadhi ushindi huu na kuendelea kujiandaa kwa michezo ijayo. Tutacheza michezo miwili ya majaribio ili kukiandaa kikosi chetu na labda tunaweza kuita wachezaji wapya ili kuongeza nguvu," alisema.

Hivi sasa, Cuperly aliongeza kuwa ameridhishwa na mwenendo wa timu hiyo katika ukabaji lakini katika ushambuliaji bado kuna kazi ya kufanya.

"Tuliweza kuzuia vizuri na bao tulilopata lilikuwa zuri. Lile bao lilitokana kwa pamoja na Chamakh na El Hamdaoui. Inabidi tubaki katika kiwango cha juu katika mechi zote za kufuzu na kufanya kazi kwa bidii ili kuwaridhisha mashabiki wetu.

No comments:

Post a Comment