Wednesday, October 13, 2010

DUNGA AMSIHI NEYMAR KUHAMIA JUVE.

BRASILIA, Brazil
KOCHA wa zamani wa Brazil Dunga amemwambia Neymar kutojiunga na Chelsea na badala yake ajiunge na klabu ya Juventus pindi atapoondoka katika klabu yake ya Santos.

Kinda huyo mwenye miaka 18, kidogo ahamie Stamford Bridge katika kipindi cha majira ya kiangazi lakini vilabu hivyo vilishindwa kukubaliana ada ya uhamisho wa machezaji huyo. Juventus wamekuwa wakimnyemelea mchezaji huyo toka kipindi hicho na Dunga anaamini kuwa ili aweze kuendelea ni bora ahamie Serie A.

"Lazima tuwe na uvumilivu kwa watu wadogo," alikaririwa Dunga na gazeti la Daily Mail.

"Lakini Juventus ni klabu inayojua umuhimu wa kutunza vipaji. Neymar bado mdogo sana lakini tayari ameshaanza kuonekana katika timu ya Taifa."

No comments:

Post a Comment