MILAN, Italia
KLABU ya soka ya Inter Milan inataka kuvamia soko la Ligi Kuu ya Uingereza na mchezaji mahiri wa Arsenal Cesc Fabrigas ndio wa kwanza wanayemuhitaji katika kipindi cha dirisha dogo Januari mwakani, alidai Pierpaolo Marino.
Bosi huyo wa zamani wa Napoli amaamini kuwa Inter wa Nerazzuri wataongeza nguvu baada ya kushindwa kutengeneza kikosi imara katika majira ya kiangazi, na wanatarajia kuhamishia nguvu zao kwa Fabrigas.
Tatizo kubwa litakalowakabili ni kuwashawishi Arsenal kummuachia mchezaji huyo. Inter pia itapata upinzani kutoka Barcelona ambayo nayo inammezea mate mchezaji huyo.
"Kama Benitez angewashawishi wakurugenzi kumsikiliza katika kipindi hicho basi wangeweza kufanikiwa katika kipindi cha mwezi August," alisema Morino.
"Fabrigas na Dirk Kuyt wa Liverpool. Kama wataweza kukamilisha taratibu za kuwanyakuwa hawa hakuna yeyote anayeweza kusema katika klabu hiyo kwani wachezaji hao watyakamilisha kikosi kilicho bora kabisa."
No comments:
Post a Comment