Tuesday, October 12, 2010

VIINGILIO SIMBA NA YANGA CCM KIRUMBA HIVI HAPA.

SHIRIKISHO la Soka nchini (TFF) limetangaza viingilio vya mchezo wa watadi kati ya timu ya Simba na Yanga mchezo utakaochezwa Octoba 16 katika Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Sunday Kayuni alisema maandalizi kwa ajili ya mchezo huo yanaendelea ambapo wenyeji wa mchezo huo itakuwa ni klabu ya Simba.

Alisema katika mchezo huo kiingilio cha juu kabisa yaani viti maalumu au VIP kitakuwa ni shilingi 30,000, eneo la jukwaa kuu kiingilio kitakuwa shilingi 20,000 wakati kiingilio cha chini kitakuwa shilingi 5,000 upande wa mzunguko.

Alisema wamefikia hatua ya kuweka viwango vya chini ili kila mkazi wa Mwanza aweze kumudu kwenda kupata burudani ambayo muda mrefu walikuwa hawajaipata ya kushuhudia timu zao zikipambana katika uwanja huo.

No comments:

Post a Comment