MADRID, Hispania
BAADA ya kufafanua kuwa rafiki yake mkubwa katika mpira ni kocha Manchester United Sir Alex Ferguson, kocha Real Madrid Jose Mourinho aliwaambia waandishi wa habari sababu zake kwanini anaipenda Uingereza kuliko nchi zingine alizowahi kufundisha.
"Hakuna mahojiano yaliyofanyika bila kunitaja mimi hapa Hispania, fikiria kama najali hili. Bora Uingereza. Nafikiri kuwa Ureno, Italia na Hispania kuna baadhi ya mashabiki huwa wanachagua siku kabla na baada ya mchezo, kuliko mchezo wenyewe," alisema Mourinho.
Mourinho aliwahi kuongea kuhusu mapenzi aliyonayo na Ligi Kuu ya Uingereza wakati akifundisha Inter na ilimfanya kutengeneza uadui kwa baadhi ya waandishi na makocha kwa kuonyesha mapenzi yake na Uingereza.
"Furaha kubwa niliyonayo kuhusu kazi na shughuli yangu ni kuwa imeniwezesha kufundisha Ureno, Uingereza, Italia na sasa Hispania. Inanifanya kuwa kocha tajiri kuliko yule ambaye amefundisha sehemu zinazofanana na utamaduni unaofanana," alimalizia Mourinho.
No comments:
Post a Comment