Tuesday, October 12, 2010
"NAFASI YANGU INAWEZA KUZIBWA," - XAVI.
BARCELONA, Hispania
KIUNGO wa Barcelona Xavi amesisitiza kuwa nafasi yake inaweza kuzibwa katika kikosi hicho na kufafanua kuwa timu yake ya Taifa ya Hispania nayo pia inafuata mfumo huohuo na kutomtegemea mchezaji mmoja.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Hispania ambaye kwa sasa anauguza majerahalakini anatarajiwa kurudi uwanjani mwishoni mwa wiki wakati timu yake itakapocheza dhidi ya Valencia katika Uwanja wa Nou Camp. Akiongea na Barca TV, Xavi alifafanua kuwa ingawa ni mchezaji wa kutegemewa katika kikosi cha Pep Guardiola, haimaanishi kuwa nafasi yake haiwezi kuzibwa.
"Hapana, hapana hapana," alisema Xavi. "Unaweza kuliona hilo siku moja. jinsi tunavyocheza ni sawasawa na haihitaji kitu au mchezaji fulani kuweza kufanyika. Ingawa, kama [Leonel] Messi hayupo huwa tunamkumbuka, kama ilivyo kwa [Andres] Iniesta, [David] Villa au [Carles] Puyol, kwasababu ni wachezaji muhimu, lakini hakuna hata mmoja mmoja wetu ambaye nafasi yake haiwezi kuzibwa."
Xavi (30) pia ameondoa minong'ono iliyopo kuhusu yeye kuwa mchezaji bora wa dunia na anaamini kuwa heshima hiyo anastahili mchezaji mwezake Messi.
"Sidanganyi, kuna mchezaji mmoja ambaye yuko katika nafasi ya juu. Naweza kusema kusema sijawahi kumuona mchezaji kama yeye katika maisha yangu.
"Ni mchezaji wa aina yake kama anavyosema Peps, anacheza sehemu zote, ana kasi, jasiri, nguvu ana kila kitu! Nadhani huwa wanakuwepo kama yeye katika kila miaka 50, kwahiyo ukitaka kuchagua aliye bora basi ni Messi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment