Monday, February 21, 2011

VILLA SQUARD YAFANIKIWA KUREJEA KATIKA LIGI KUU BARA.

TIMU ya Villa squad yenye makazi yake jijini Dar es Salaam imefanikiwa kurejea katika Ligi kuu ya soka Tanzania baada ya kutoka suluhu na timu ya Prisons ya Mbeya katika mchezo wa Ligi ya Daraja la Kwanza uliofanyika katika Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Villa Squad imefikisha pointi 12 sambamba na Polisi Morogoro, lakini timu hiyo ya Magomeni iliyoshuka daraja mwaka 2009, inafaida ya tofauti ya magoli, ambapo ina magoli 12 ya kufunga dhidi ya magoli 8 ya Polisi Moro.

Msemaji wa Villa Idd Godigodi akiwa mwenye furaha, amesema klabu hiyo imefurahi kurejea tena katika Ligi Kuu, na kuwa hayo ni mafanikio makubwa kwa klabu kwa kuwa imeandika historia mpya ya kujivunia

No comments:

Post a Comment