Thursday, March 24, 2011

ALVES AONGEZEWA MKATABA BARCA.

BARCELONA, Hispania
BEKI wa pembeni wa kimataifa toka nchini Brazil Daniel Alves amekubalia kusaini mkataba mpya wa kuendelea kuwatumikia mabingwa wa soka nchini Hispania FC Barcelona.

Alves amekubali kusaini mkataba huyo baada ya kueleza wazi mipango yake mara baada ya msimu huu kumalizika ambapo maamuzi aliyotaka kuyachukua ni kuihama klabu hiyo ya nchini Hispania na kusaka klabu nyingine huku tegemeo lake kubwa likiwa Man City.

Mkataba utakaosainiwa na beki huyo mwenye umri wa miaka 27 utamuwezesha kuendelea kuitumikia Barcelona hadi mwezi June mwaka 2015.

Mbali na kueleza mipango yake ya kutaka kuondoka klabuni hapo mwishoni mwa msimu huu pia mchezaji huyo alionyesha kuchukizwa na hatua ya viongozi wa Barca ambao hawakumuonyesha ushirikiano wa kutosha wa kumthibitishia kama wapo tayari kukaa nae mezani na kumaliza mara moja suala hilo.

Alves alisajiliwa na Fc Barcelona mwishoni mwa msimu wa mwaka 2007-08 akitokea Sevilla na tayari ameshaitumikia klabu hiyo ya Catalunya katika michezo 141.

No comments:

Post a Comment