KIUNGO wa klabu ya Bayer Leverkusen Michael Ballack amelazimika kuomba radhi kupitia mtandao wa klabu hiyo kufuatia kulishawishi kundi la mashabiki wa Factory Squad kutoa maneno makali kwa mashabiki wa mjini Cologne waliokua wamehudhuria kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Schalke 04 mwishoni mwa juma lililopita.
Ballack alitoa maneno makali kwa mashabiki hao baada ya kikosi cha Bayer Leverkusen kupata ushindi wa mabao mawili kwa sifuri kwenye uwanja wa BayArena ambapo alidiriki kufanya hivyo kwa kutumia kipaza sauti.
Alisema anajutia kosa alilolifanya na hana budi kusamehewa kutokana na mazingira yaliyokuwepo uwanjani hapo baada ya kikosi chao kufanikiwa kuzipata point tatu muhimu.
Kitendo hicho kilichofanywa na Ballack huenda kikaishawishi kamati ya nidhamu ya chama cha soka nchini Ujerumani kumuadhibu kiungo huyo ambae bado msaada wake unahitajika katika kipindi hiki cha kuelekea mwishoni mwa ligi.
No comments:
Post a Comment