KOCHA wa kimataifa toka nchini Ureno pamoja na klabu ya Real Madrid ya nchini Hispania José Mourinho, ameendelea kusisitizia jambo la kurejea tena nchini Uingereza kuitumikia moja ya klabu kubwa inayoshiriki ligi kuu.
Mourinho ameendelea kutoa msisizo huo alipohojiwa na shirika la utangazaji la nchini Uingereza BBC ambapo alisema dhamira hiyo inatokana na kuyapenda sana maisha ya nchini humo ambapo aliishi kwa muda wa miaka minne akiwa na kikosi cha klabu ya Chelsea.
Alisema kwa sasa ni vigumu kueleza wazi ni lini anatarajia kurejea nchini Uingereza kutokana na mkataba wa miaka minne alioingia na uongozi wa klabu ya Real Madrid mwishoni mwa msimu uliopita lakini ukweli ni kwamba baada ya kuondoka nchini Hispania hatokwenda popote zaidi ya kurejea kwenye himaya ya malkia Elizabeth.
Mourinho pia amzungumzia hatua ya kikosi chake kupangwa na klabu ya Tottenham Hotspurs kwenye mchezo wa hatua ya robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya ambapo alisema hakujihisi vibaya bali alilipokea suala hilo kwa mikono miwili.
Alisema aliomba usiku na mchana kutosikia wala kuona anapangwa na klabu ya Chelsea ama Inter Milan na endapo ingetokea hivyo angekua na mazingira magumu sana kutokana na mapenzi yeke dhidi ya klabu hizo mbili ambazo amezipa mafanikio makubwa.
Hata hivyo Mourinho ameeleza kwamba Tottenham Hotspurs ni klabu yenye ushindani na imeleta changamoto mpya kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya baada ya kufanikiwa kuzifunga klabu za mjini Milan ambazo ni Inter Milan pamoja na AC Milan.
Katika hatua nyingine meneja huyo alisema ana uhakika kiungo wa kikosi chake toka nchini Ureno Cristiano Ronaldo ambae mwishoni mwa juma lililopita alijitonesha maumivu ya nyama za paja atauwahi mchezo huo wa hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya utakaochezwa mwanzoni mwa mwezi ujao.
No comments:
Post a Comment