MSHAMBULIAJI wa kimataifa toka nchini Denmark na klabu ya Arsenal Nicklas Bendtner hii leo amelazimika kurejeshwa kambini baada ya kuumia akiwa katika maandalizi na wachezaji wenzake wa timu ya taifa kabla ya mpambano wa mwishoni mwa juma hili dhidi ya timu ya taifa ya Norway.
Bendtner amefikia hatua hiyo kufuatia kuumia kifundo cha mguu wake wa kulia na taarifa zaidi juu ya jeraha linalomkabili zitatolewa baadae baada ya majibu ya vipimo vya picha za x-Ray kueleza wazi.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 23 amefikwa na maswahibu hayo alipokua kwenye heka heka za kukimbia mbio za kawaida kabla ya kujiunga wachezji wengine tayari kwa mazoezi kamili toka kwa kocha mkuu wa timu ya taifa ywa Denmark Morten Olsen.
Kuumia kwa, Bendtner kunaendelea kuzua hofu kwa klabu yake ya Arsenal ambayo ipo kwenye nafasi nzuri ya kuwanai taji la ligi kuu ya soka nchini Uingereza msimu huu kufautia utofauti wa point nne uliopo kati ya The Gunners dhidi ya Man Utd.
No comments:
Post a Comment