NAHODHA na kiungo wa timu ya taifa ya Uholanzi Mark van Bommel hatojumuishwa kwenye kikosi kitakacho endelea na kampeni ya kusaka nafasi ya kucheza fainali za mataifa ya barani Ulaya za mwaka 2012 kwa kucheza na timu ya taifa ua Hungary mwishoni mwa juma hili kutokana na sababu za kuwa majeruhi.
Van Bommel ataukosa mchezo huo wa kundi la tano kufuatia jeraha la paja linalomsumbua kwa sasa lakini bado imeelezwa ataendelea kusalia kambini kwa ajili ya mchezo wa March 29 ambapo Uholanzi watakua nyumbani wakirejeana na timu ya taifa ya Hungary.
Wachezaji wengine wa timu ya taifa ya Uholanzi ambao tayari wameshatemwa kikosini kufautai sababu za kuwa majeruhi ni pamoja na Arjen Robben, Klaas Jan Huntelaar pamoja na Hedwiges Maduro.
No comments:
Post a Comment