KIUNGO wa klabu bingwa barani Ulaya Inter Milan ambae anaitumikia klabu ya Sunderland ya nchini Uingereza kwa mkopo Suleyman Muntari amezusha hofu kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Ghana kinachojiandaa na mchezo wa kuwania nafasi ya kucheza fainali za mataifa ya bara la Afrika kwa kucheza na timu ya taifa ya Congo Brazzaville pamoja na mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya Uingereza.
Kiungo huyo amezusha hofu hiyo baada ya kuumia kiazi cha mguu mwishoni mwa juma hili alipokua kwenye mchezo wa ligi ambapo Sunderland walikubali kisago cha mabao 2-0 toka kwa Liverpool huko Stadium of Lights.
Tayari meneja wa klabu ya Sunderland Steve Bruce ameshaeleza kwamba hadhani kama kiungo huyo atakua na nafasi ya kutosha ya kucheza michezo ya kimataifa kwa katika kipindi hiki cha juma moja na nusu.
Katika hatua nyingine kocha mkuu wa timu ya taifa ya Ghana Goran Stevanovic, amejiandaa kuikabili timu ya taifa ya Uingereza pasipokua na kiungo wa klabu ya Chelsea Michael Essien ambae ameweka msimamo wa kutokua tayari kurejea katika kikosi cha timu ya taifa kwa sasa.
Hata hivyo kocha huyo bado anaamini Essien atabadili msimamo huo na kurejea kwenye kikosi cha timu ya taifa lake ambacho hajawahi kukitumikia kwa muda wa mwaka mmoja sasa.
No comments:
Post a Comment