UONGOZI wa klabu ya Lazio ya nchini Italia unaaminikikosi chao kina uwezo mkubwa ya kujihakikishia nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa msimu ujao bila ya kuwa na kiungo wa kimataifa toka nchini Brazil Matuzalém Francelino da Silva.
Imani hiyo kwa viongozi wa Lazio imekuja baada ya Silva kuongezewa adhabu na kamati ya nidhamu ya Chama cha Soka nchini Italia kufuatia kosa alilolifanya katika mchezo wa mwishoni mwa juma lililopita dhidi ya Cecena waliokubali kisago cha bao 1-0 kilichotolewa huko Stadio Olympico.
Kamati ya nidhamu ya chama cha soka nchini Italia imetoa taarifa za kumuongezea adhabu kiungo huyo kutoka mchezo mmoja hadi mitatu baada ya kufuatilia picha za televisheni za mchezo huo na kubainika kwamba Silva alimsukuma kwa makusudi kiungo wa klabu ya Cecena Antonio Jimenez pindi timu hizo zipokutana mwishoni mwa juma lililopita.
Kwa sasa Lazio wanakamata nafasi ya tano kwenye msimamo wa ligi ya nchini Italia kwa kufikisha point 54 huku michezo minane ikisalia.
Kamati ya nidhamu ya chama cha soka nchini Italia pia imethibitisha kwamba beki wa kimataifa toka nchini Brazil na klabu ya Inter Milan Lucio hatocheza mchezo ligi utakaomua nani ataelekea kileleni kati ya mahasimu wawili wa jiji la Milan AC Milan dhidi ya mabingwa watetezi.
Lucio ataukosa mchezo huo wa April mbili kufuatia kadi ya njano aliyoonyeshwa mwishoni mwa juma lililopita kwenye mchezo dhidi ya Lecce hali ambayo inamfanya kuwa na kadi tano za njano.
No comments:
Post a Comment