Wednesday, March 23, 2011

UCHAGUZI FIFA: BLATTER KUACHIA NGAZI 2015, BIN HAMMAN AKALIA KOONI.

NYON, Switzerland
RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Sepp Blatter amepanga kuachia ngazi mwaka 2015 endapo atachaguliwa kuliongoza shirikisho hilo katika uchaguzi wa mwezi June mwaka huu.

Blatter mwenye umri wa miaka 75 ametoa msimamo huo alipopata nafasi ya kuhutubia kwenye mkutano wa Shirikisho la Soka barani Ulaya (UEFA) unaofanyika mjini Nyon nchini Uswis.

Alisema endapo atapa kipindi kingine cha miaka minne cha kuiongoza FIFA atakua na umri mkubwa zaidi hivyo hatokua na budi kuachia nafasi kwa wengine waendeleze pale atakapoachia.

Mohamed Bin Hamman.
Hata hivyo kiongozi huyo ambae aliingia madarakani mwaka 1998, tayari anakabiliwa na upinzani wa hali ya juu kutoka kwa raisi wa Shirikisho la Soka barani Asia Mohamed Bin Hammam alitangaza dhamira hiyo mwishoni mwa juma lililopita.

Suala kubwa linalopigiwa upatu na Mohamed Bin Hammam ambalo linachukuliwa kama sehemu inayomtia hofu kwa Blater ni usiri mkubwa uliokithiri ndani ya FIFA ambao unatakiwa kukomeshwa na uongozi wa mdau huyo wa soka kutoka nchini Qatar endapo atachaguliwa.


Akihojiwa Hammam alisema wadau wa soka ulimwenguni kote wanastahili kufahamu suala lolote linaloendelea ndani ya FIFA pasipo kufichwa na hivyo utawala wake utahakikisha unalitimiza hilo na kuondoa dhana ya kuongoza mpira kama ilivyo katika Nyanja za siasa.

Alisema jibu kubwa ya kumaliza mzozo huo ni kuundwa kwa kamati ya kuweka masuala mbali mbali hadharani ambayo itakua ikifanya kazi yake bila kwa kwenda sambamba na tukio husika aidha liwe la faida ama hasara ndani ya FIFA.


No comments:

Post a Comment