WINGA wa klabu ya Wolves Hampton Wanderers Matt Jarvis amefanikiwa kuitwa kwa mara ya kwanza kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza ambacho juma hili kitaingia kambini kujiandaa na mchezo wa kuwania nafasi ya kucheza fainali za mataifa ya bara la Ulaya dhidi ya timu ya taifa ya Wales na kisha mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi yua timu ya taifa ya Ghana.
Winga huyo mwenye umri wa miaka 24 ameitwa kikosini na kocha mkuu wa timu ya taifa ya Uingereza was Fabio Capello kufuatia kuumia kwa winga wa klabu ya Arsenal Theo Walcott pamoja na Adam Johnson wa klabu ya Man City.
Hata hivyo kuitwa kwa Matt Jarvis bado kunatoa changamoto kwa mawinga wengine waliojumuishwa kwenye kikosi hicho chenye wachezaji 26, Aaron Lennon pamoja na Ashley Young ambao huenda wakaanzishwa katika kikosi cha kwanza.
Mtandaji mkuu wa klabu ay Wolves Hampton Wanderers Jez Moxey amesema wamefurahishwa na kitendo cha mchezaji huyo kuitywa kwenye kikosi cha timu ya taifa hatua mbayo wanaichukuliwa kama sehemu ya kukua kwa klabu yao licha ya kuendelea kuburuza mkia kwenye msimamo wa ligi.
Nae mshambuliaji mpya wa klabu ya Liverpool Andy Carroll, ameitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza baada ya kupona jeraha la paja ambapo kwa mara ya kwanza aliichezea timu hiyo kwenye mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya Ufaransa mwezi Novemba mwaka jana.
Kikosi kamili cha Uingereza upande wa:
Makipa: Joe Hart (Manchester City), Ben Foster (Birmingham City), Robert Green (West Ham United)
Mabeki: Glen Johnson (Liverpool), John Terry (Chelsea), Phil Jagielka (Everton), Ashley Cole (Chelsea), Kyle Walker (Tottenham Hotspur - on loan at Aston Villa), Gary Cahill (Bolton Wanderers), Michael Dawson (Tottenham Hotspur), Joleon Lescott (Manchester City), Leighton Baines (Everton)
Viungo: Aaron Lennon (Tottenham Hotspur), Jack Wilshere (Arsenal), Frank Lampard (Chelsea), Ashley Young (Aston Villa), James Milner (Aston Villa), Scott Parker (West Ham United), Gareth Barry (Manchester City), Stewart Downing (Aston Villa), Matthew Jarvis (Wolverhampton Wanderers)
Washambuliaji: Andy Carroll (Liverpool), Wayne Rooney (Manchester United), Darren Bent (Aston Villa), Peter Crouch (Tottenham Hotspur), Jermain Defoe (Tottenham Hotspur)
No comments:
Post a Comment