Tuesday, March 22, 2011

CR7 HATIHATI KUIVAA TOTTENHAM CHAMPIONS LEAGUE.

MADRID, Hispania
KIUNGO wa kimataifa toka nchini Ureno pamoja na klabu ya Real Madrid Cristiano Ronaldo atakua nje ya uwanja kwa muda wa majuma matatu yajayo kufuatia majeraha ya nyama za paja aliyoyapata katika mchezo wa mwishoni mwa juma lililopita.

Kiungo huyo alilazimika kutolewa nje ya uwanja katika mchezo wa ligi dhidi ya Atletico Madrid waliokubalia kisago cha mabao mawili kwa moja na nafasi yake ilichukuliwa na muagentina Angel De Maria.

Kuumia kwa Cristiano Ronaldo kunamaanisha hatokuwepo kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Ureno ambacho mwishoni mwa juma hili kitacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya Chile na kisha kitarejea kwenye kampeni ya kusaka tiketi ya kucheza fainali za ulaya za mwaka 2012 kwa kuonyeshana undava na timu ya taifa ya Finland.

Mbali na kutokuwepo katika michezo hiyo ya kimataifa Cristiano Ronaldo pia amezua hofu kubwa ya kutokuwepo katika kikosi cha Real Madrid ambacho kitacheza mchezo wa hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya dhidi ya Tottenham Hotspur April 5 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment