MUNICH, Ujerumani
KOCHA Mkuu wa timu ya taifa ya nchi hiyo Joachim Loew amemtema kiungo na nahodha wake Michael Ballack kwenye kikosi kitakachoanza maandalizi mwanzoni mwa juma lijalo tayari kwa kuendelea na kampeni ya kusaka nafasi ya kucheza fainali za Mataifa ya Bara la Ulaya za mwaka 2012.
Loew ametangaza kumtema kiungo huyo mwenye umri wa miaka 34 baada ya kushindwa kurejea katika hali yake ya kawaida kama ilivyokua ikitarajiwa kufuatia maumivu ya mfupa wa ugoko aliyoyapata mwanzoni mwa msimu huu.
Alisema pamoja na kumtema kwenye kikosi chake ambacho kitacheza na timu ya taifa ya Kazakhstan, pamoja na Australia bado anatarajia kuketi nae chini kwa lengo la kujadili mustakabali wa maisha yake ya baadae ndani ya kikosi cha Ujerumani ambacho kilimaliza katika nafasi ya tatu kwenye fainali za kombe la dunia.
Katika kikosi cha Ujerumani Loew amemrejesha kikosini kiungo wa klabu ya Bayern Munich Toni Kroos pamoja Mario Gomez ambao wote kwa pamoja waliukosa mchezo wa mwezi Februali dhidi ya timu ya taifa ya Italia kufuatia sababu za kuwa majeruhi.
Pia amemuita mshambuliaji wa klabu ya Mainz Andre Schuerrle, ambae alianza kuitumikia timu ya taifa ya Ujerumani mwaka jana huku kipa wa Werder Bremen Tim Wiese nae akichukuliwa kama kipa chaguo la tatu.
Kikosi kamili cha Ujerumani kwa upande wa;
Makipa: Manuel Neuer (Schalke 04), Rene Adler (Bayer Leverkusen), Tim Wiese (Werder Bremen);
Mabeki: Arne Friedrich (VfL Wolfsburg), Dennis Aogo (Hamburg SV), Holger Badstuber (Bayern Munich), Philipp Lahm (Bayern Munich), Jerome Boateng (Manchester City), Mats Hummels (Borussia Dortmund), Per Mertesacker (Werder Bremen), Marcel Schmelzer (Borussia Dortmund);
Viungo: Mario Goetze (Borussia Dortmund), Sven Bender (Borussia Dortmund), Mesut Ozil (Real Madrid), Sami Khedira (Real Madrid), Bastian Schweinsteiger (Bayern Munich), Christian Traesch (VfB Stuttgart), Toni Kroos (Bayern Munich), Andre Schuerrle (Mainz 05)
Washambuliaji: Mario Gomez, Miroslav Klose, Thomas Mueller (all Bayern Munich), Lukas Podolski (Cologne)
No comments:
Post a Comment