KOCHA Mkuu wa mabingwa wa soka duniani Hispania Vicente del Bosque, amemuita kikosini mshambuliaji wa klabu ya Valencia Juan Manuel Mata García pamoja na kiungo wa klabu ya Osasuna Javier "Javi" Martínez Aguinaga kwa ajili ta mchezo wa kuwania nafasi ya kucheza fainali za mataifa ya barani Ulaya za mwaka 2012.
Del Bosque amewaita kikosini wachezaji hao kwa lengo la kuziba mapengo yaliyoachwa wazi na wachezaji majeruhi ambapo kwa upande wa Juan Manuel Mata García ataziba nafasi ya mshambuliaji wa klabu ya Barcelona Pedro huku Javier "Javi" Martínez Aguinaga akitarajiwa kuziba nafasi ya kiungo wa klabu ya Arsenal Cesc Fabregas.
Beki wa klabu ya Athletic Bilbao Andoni Iraola nae amejumuishwa kikosini baada ya kukosekana kwa beki na nahodha wa klabu ya Barcelona Carles Puyol ambae bado anasumbuliwa na maumivu ya mguu wake wa kulia.
Kikosi kamili cha Hispania kilichoitwa hii leo kwa upande wa;
Makipa: Iker Casillas (Real Madrid), Victor Valdes (Barcelona), Pepe Reina (Liverpool).
Mabeki: Alvaro Arbeloa (Real Madrid), Sergio Ramos (Real Madrid), Raul Albiol (Real Madrid), Gerard Pique (Barcelona), Carlos Marchena (Villarreal), Joan Capdevila (Villarreal), Andoni Iraola (Athletic Bilbao).
Viungo: Xavi (Barcelona), Xabi Alonso (Real Madrid), Andres Iniesta (Barcelona), Javi Martinez (Athletic Bilbao), Sergio Busquets (Barcelona), Santi Cazorla (Villarreal).
Washambuliaji: David Silva (Manchester City), David Villa (Barcelona), Fernando Torres (Chelsea), Fernando Llorente (Athletic Bilbao), Jesus Navas (Sevilla), pamoja na Juan Mata (Valencia).
Kikosi cha tumu ya taifa ya Hispania mwishoni mwa juma lijalo kitaendelea na kampeni ya kusaka nafasi ya kutetea ubingwa wa barani ulaya kwa kucheza na timu ya taifa ya jamuhuri ya Czech nyumbani na kisha kitasafiri siku nne baadae kucheza na kwa ajilia ya kucheza na timu ya taifa ya Lithuania.
No comments:
Post a Comment