SHIRIKISHO la Soka barani Ulaya (UEFA) kupitia kamati yake ya nidhamu limetangaza kumfungia michezo mitatu kiungo wa kimataifa toka nchini Italia pamoja na klabu ya AS Roma Daniele de Rossi baada ya kumbaini alifanya kosa ambalo halikutiliwa maanani na muamuzi.
Rossi amefikwa na adhabu hiyo baada ya picha za televisheni za mchezo wa marejeano wa hatua ya 16 bora ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya kati ya AS Roma dhidi ya Shakter Doneski kuonyesha kuwa alimpiga kiwiko nahodha wa klabu hiyo ya nchini Ukraine Darijo Srna.
Katika taarifa iliyotolewa na kamati ya nidhamu ya UEFA imeeleza kwamba Rossi alifanya kitendo hicho kwa makusudi na hakuadhibiwa na muamuzi alichezesha mchezo huo kutokana na mazingira yaliyokuwepo uwanjani hapo.
Katika mchezo huo wa marejeano uliochezwa mjini Doneski nchini Ukraine wenyeji walipata ushindi wa mabao matatu kwa sifuri ambao uliwawezesha kutinga katika hatua ya robo fainali ambayo itawakutanisha na mabingwa wa soka nchini Hispania Fc Barcelona.
No comments:
Post a Comment